1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaIran

Marekani yaitaka Iran kutowapa silaha waasi wa Houthi

14 Mei 2024

Marekani imeitolea mwito Iran kutowapa silaha wapiganaji wa kundi la waasi wa Kihouthi, silaha ambazo wanazitumia kufanya mashambulizi dhidi ya meli katika bahari ya Sham na sehemu nyengine.

https://p.dw.com/p/4fokG
Askari wa kikosi cha Houthi wanaoungwa mkono na Iran
Askari wa kikosi cha Houthi wanaoungwa mkono na IranPicha: Osamah Yahya/dpa/picture alliance

Naibu balozi wa Marekani Robert Wood katika Umoja wa Mataifa ameliambia Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuwa, iwapo inataka kufanikiwa kumaliza vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini Yemen basi haina budi kuionya Iran.

Wood ameeleza kuwa, Iran haiwezi kuendelea kujificha nyuma ya kivuli cha Wahouthi.

Soma pia: Marekani yashambulia maeneo ya Wahotuhi wa Yemen

Mwanadiplomasia huyo amesema kuna ushahidi wa kutosha kwamba Iran inawapa wapiganaji wa Kihouthi silaha za kisasa, hatua ambayo ni ukiukaji wa vikwazo vya Umoja wa Mataifa.

Marekani imesema kuwa wapiganaji wa Kihouthi wamefanya zaidi ya mashambulizi 50 dhidi ya Meli, wameikamata meli moja na kuizamisha nyengine tangu mwezi Novemba.